Tunanuia kuwapa vijana nafasi nzuri ya kukua kimaadili, kiali na kimwili chini ya misingi thabiti ya upendo na taaluma iliyotukuka.
(Education for a future of hope)
Kujenga msingi wa nidhamu, kiroho na upendo kwa kila mtoto bila ubaguzi.
Kuhakikisha kila mwanafunzi anafikia ufaulu wa hali ya juu na kujitegemea.
Kuwasaidia na kuwajumuisha watoto wote pasi na ubaguzi kupata elimu na usawa kijamii.
Shule ya Maria De Mattias imeanzishwa kwa kusudi la kuwapa vijana nafasi nzuri ya kukua kimaadili, kiali na kimwili.
Maria De Mattias, mwanzilishi wa Shirika la Masista Waabuduo Damu ya Kristo (wanaomiliki shule), alikuwa na upendo mkuu kwa vijana. Aliamini kuwa kwa njia ya elimu kila kiumbe anaweza kumwelewa zaidi Mungu na maana ya maisha.
Zaidi ya hayo, shule hii imejengwa kwa ajili ya kupokea watoto wote pasi na ubaguzi ili waweze kupewa elimu kama ufunguo wa maisha na kuwarejesha katika mazingira ya kawaida kijamii.
Tunaweka viwango vya juu vya mahadhurio, ufaulu na nadharia kwa mazingira halisi.
Kutoa Elimu bora kwa watoto wote kwa kuhakikisha kila mtoto anafikia kiwango cha juu cha kuelewa na kufaulu ili aweze kujitegemea kimaadili, kiuchumi na kijamii kama nafsi na Taifa kwa ujumla.
"Elimu kwa kizazi chenye matumaini"
(Education for a future of hope)
Pata fomu za kujiunga na maelezo ya kina ya shule hapa.
Tazama picha za matukio mbalimbali, masomo na mazingira ya shule yetu.
Picha zitapakitiwa hivi karibuni.
Tupo tayari kupokea maswali yako kuhusu usajili, nafasi za masomo na ushirikiano.
Maria De Mattias Pre & Primary School
P.O. Box 511 Dodoma, Tanzania
+255 757 100 888
Jaza fomu hii kuwasiliana nasi moja kwa moja kwa usaidizi wa haraka.